UWAKILI
UTANGULIZI
Kuna maeneo ambayo Mungu ametupa kuwa mawakili kwayo na ambayo tunatakiwa kuwa waaminifu. Maeneo haya ni haya yafuatayo:
1. Muda: Muda ni mtaji ambao Mungu ametupa ili tuutumie vizuri. Nadiriki kusema katika mitaji yote ambayo mtu aweza kuifikiria, hakuna mtaji wa maana zaidi kuliko muda. Tofauti kati ya maskini na tajiri iko katika jinsi ambavyo kila mmoja wao anavyoutumia muda wake. Kuna wengine ambao wanasema, „ Aaa, niko hapa bwana, napoteza muda!..." Muda ukisha potea haiwezekani kuupata tena. Hata ungalipanda chombo chenye uwezo wa kwenda kasi kuliko kasi ya nuru isafiripo, bado hutaweza kuupata muda uliokwisha potea. Ni vyema usipoteze muda. Nadiriki kusema kwamba wakazi wan chi za Magharibi wamewashinda wakazi wa nchi zinazoitwa zinaendelea kwa jinsi ambavyo wanatumia muda wao kwa umakini na uuangalifu mno. Mke wangu, ambaye ni mtu kutoka katika nchi mojawapo ya magharibi, amenisaidia kuona umuhimu wa kuto[poteza muda. Kwa mfano, ameweka vijigazeti na vijitabu chooni ili hata muda ule ambao mtu anakuwa anajisaidia chooni aweze kuutumia kwa kusoma! Bila shaka pia umeona watu wengine ambao watumia muda wao wawapo katika basi ama mahali pengine pa kusubiri kwa manufaa, mfano kwa kusoma, hata kama ni katika daladala! Biblia inatufundisha kuutumia muda wetu vyema. Zaburi 90: 12: "Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima" Efeso 5: 15 - 16: "Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima, bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu" Wekeza ("invest") muda wako katika vitu na mambo ya maana, yadumuyo milele. Kuna mambo yasiyo dumu, na kuna mambo yadumuyo milele. Mimi nakushauri uwekeze muda wako katika mambo yadumuyo milele. Mifano ya mambo yadumuyo milele ni:
Vipaji tulivyopewa na Mungu Mfano Mwili, Ujuzi, Hekima nk. "Usimwue farasi kabla hajafikisha ujumbe" Usiuwe mwili wako kabla hujafikisha ujumbe {Injili} Pata muda wa kupumzika Fanya mazoezi N.k Nafasi tulizonazo katika jamii Tumia nafasi uliyo nayo kwa hekima Ester alitumia nafasi aliyo kuwa nayo kuwaokoa Israel pia Yusufu alitumia nafasi aliyo kuwa nayo katika jamii kuwasaidi ndugu zake ambao walikuwa hawana chakula Karama za kiroho -1korinto 12: 4 -7 3 Hazina zetu: Uwe maskini uwe Tajiri unaitaji kuelewa kanuni za Baraka zifuatazo:- a} Kanuni ya kurejeshewa Luka 6:38 Mithali 11:24-31 {Zaburi 41:1-3} 2Wakorinto 9:6 Mithali 19:17 b} Kanui ya kulinganisha kiwango na kipato: - Luka 21:1-4 Kanuni ya kutoa kwa moyo wa furaha. 2 kor 9:7 Kanuni ya baraka toka juu 2 kor 8 - 11 Kanuni ya kupokea toka kwa wengine toka kwa wengine pale unapokuwa mhitaji. 2 kor 8 - 15. Fedha. Kuna kanuni za kimungu za kukufanya uwe wakili mwaminifu kwa habari ya fedha.
Bwana anaagiza tutoe zaka (kikumi) Lawi 27:30-33 , malimbuko (Mithali 3:9) kumb 14:22 Katika Agano jipya, Bwana Yeu aliagiza Luka 11:42, Math 23:23 Kanuni ya kikumi 10% ya mapato yako kabla ya makato. Kikumi katika agano la kale kilitumika Kuwatunza maskini na wahitaji katika israel Kutoka 23:11 Kuwatunza walawi Kumb. 18 1 - 5 Agano Jipya Kuwaatunza maskini Mdo 4 : 34 - 37 Rum 15:26-27 Kuwatunza wahubiri na waalimu Galatia 6:6 1 Kor 9:14 Waf 4:15-18 Luka10:7 Mambo ya kukumbuka. Sisi ndio tunaoamua tubarikiwe kiasi gani Luka 6:38 Mal3:7-10 Mdo 20:35 Unachopanda ndicho unachovuna Galatia 6:7 Kutumia mali zetu kwa ajili ya Mungu ni kuwekeza Luka 12:33 Mungu ndiye akupaye nguvu za kutajirika Kumb 8:18 Mungu ndiye mwenye mali zote na vitu vyote ni vyake Zab 24:1 HITIMISHO. Hab 3:2 Labda unamwitaji Mungu afufue utoaji uliolufa katika Maisha yako. Mungu ni Mwingi wa rehema. 1. Vipawa vyetu na karama: 2. Hazina zetu: ![]() Na Mch. Lusekelo Mwaipyana |
All Content © 2003 Gospel Power Center Muta + Uswege Designs |